INJILI SONGS

Mteteeni Yesu

Mteteeni Yesu, Mlio askari
Inueni beramu, Mukae tayari
Kwenda naye vitani, Sisi hatuchoki    
Hata washindwe pia, Yeye amiliki.    

Mteteeni Yesu, Vita ni vikali;
Leo siku ya Bwana, Atashinda kweli
Waume twende naye, Adui ni wengi,
Lakini kwake Bwana, Tuna nguvu nyingi. 

Mteteeni Yesu, Wenye ushujaa;
Nguvu zenu za mwili, Hazitatufaa;
Silaha ya injili, Vaeni daima;
Kesheni Mkiomba, Sirudini nyuma,   

Mteteeni Yesu, vita ni vikali
Wengi  wamdharau, Hawamkubali;   
Ila atamiliki, Tusitie shaka;
Kuwa naye vitani, Twashinda hakika


PANDA ASUBUHI

Panda asubuhi mbegu ya fadhili,
 Panda adhuhuri, tena jioni;
Tutaingojea siku ya mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno

 Leta mavuno, leta mavuno, 
Tutafurahi kuleta mavuno;  
Leta mavuno, leta mavuno 
Tutafurahi kuleta mavuno.   

Na panda mwangani, tena kivulini,
Usiwe na hofu kwa baridi mkuu;.
Na mwisho wa kazi kuvuna mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno.        

Mvunieni Bwana kwa machozi  mengi,
Ijapo twaona taabu nyingi; mwisho wa
Kiliyo tutakaribishwa 
Tutafurahi kuleta mavuno


Comments

Popular posts from this blog

PRAISES